Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji wa Darfur kufadhiliwa misaada ya dharura na UNHCR

Wahamiaji wa Darfur kufadhiliwa misaada ya dharura na UNHCR

Ron Redmond, Msemaji wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR), aliwaambia waandishi habari mjini Geneva Ijumanne kwamba UM unaendelea kutoa misaada ya dharura kwa wahamiaji wa Darfur Magharibi waliomiminikia maeneo ya Birak na Sorok, Chad mashariki katika siku za karibuni wakikimbia mapigano. UNHCR imeripoti kwamba itawapeleka wale wahamiaji waliodhoofika kwenye kambi za Kounoungou iliopo mbali na mipaka na Sudan. Takwimu za UNHCR zimethibitisha kwamba kuanzia mwezi Februari wahamiaji wa Darfur Magharibi 13,000 walisajiliwa kuingia Chad kutoka Sudan.