Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU kuamrisha vikwazo ziada dhidi ya Iran

BU kuamrisha vikwazo ziada dhidi ya Iran

Baraza la Usalama Ijumatatu alasiri lilikutana kushauriana juu ya suala la udhibiti bora wa silaha za nyuklia duniani. Baada ya mashauriano kumalizika, wajumbe wa Baraza walijadilia mradi wa Iran unaohusu usafishaji wa madini ya yuraniamu halisi, kutumiwa katika uzalishaji wa nishati ya nyuklia. Wajumbe waliafikiana kupitisha azimio jipya, nambari 1803 (2008) ambalo liliamrisha kuanzishwa duru nyengine ya vikwazo dhidi ya Iran, kwa sababu ya Iran kukataa kusitisha mradi wa kuzalisha nishati ya nyuklia kama ilivyoidhinisha Baraza.