Rwanda yakubali kupokea wahalifu waliohukumiwa na ICTR
Mapema wiki hii mjini Kigali, Adam Deng, Msajili wa Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, walitia sahihi maafikiano ya kupeleka kifungoni kwenye magereza ya Rwanda wale watu waliohukumiwa adhabu na Mahakama. Rwanda itakuwa ni taifa la saba kuidhinisha huduma ya kuweka vizuizini wale watu waliohukumiwa na Mahakama ya ICTR kushiriki kwenye jinai ya halaiki katika Rwanda.