Hali katika Kenya na Usomali yasailiwa na BU
Ijumatano Baraza la Usalama lilikutana kushauriana hatua za kuchukuliwa na jumuiya ya kimataifa ili kurudisha utulivu na amani katika Usomali. Kadhalika Baraza lilisailia hali, kwa ujumla, nchini Kenya baada ya wajumbe wa taasisi hiyo kusikiliza fafanuzi ya ripoti ya Haile Menkerios, Msaidizi wa KM juu ya Masuala ya Kisiasa. ~~~