Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhamisho wa dharura bado waendelea Mogadishu

Uhamisho wa dharura bado waendelea Mogadishu

William Paton, Mshauri Mkaazi wa UM kuhusu Misaada ya Kiutu kwa Usomali ameripoti kuwa na wasiwasi juu ya hali ya raia 200,000 waliong’olewa makwao kutoka mji wa Mogadishu kwa sababu yaukosefu wa sualama. Kwa mujibu wa takwimu za UM, katika Januari na Februari mwaka huu wahamiaji 25,000 walikuwa wakihajiri mji kila mwezi na kumiminikia kwenye barabara inayoelekea eneo la Afgooye, ambapo kumefumka makazi ya muda ya huku na kule zaidi ya mia moja.