Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hapa na pale

Hapa na pale

Ofisi ya Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu Geneva, imetangaza ya kuwa Louise Arbour ameamua kustaafu mwezi Juni atakapomaliza miaka minne ya mkataba wake wa kazi. Arbour angelipendelea kuendelea kuongoza ofisi hiyo, na kuwakabili kinaga naga wale wakosoaji dhidi yake, lakini alisema anaaamini wakati umefika kushughulikia zaidi mahitaji ya familia yake sasa hivi.