Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Usomali kupwelewa kuandikisha watoto wa skuli za msingi, imeonya UNICEF

Usomali kupwelewa kuandikisha watoto wa skuli za msingi, imeonya UNICEF

Veronique Taveau, Msemaji wa UNICEF mjini Geneva aliwaambia waandishi habari Ijumaa kwamba taifa la Usomali lina sifa mbaya ya uandikishaji mdogo kabisa wa watoto wanaohudhuria skuli za msingi, hususan watoto wa kike. Hivi sasa imebainishwa kwamba idadi ya watoto wa kike wanaohudhuria skuli za msingi nchini ni 121,000. UNICEF impenedekeza idadi hiyo iongozwe mara mbili katika 2009 na wanalenga kuwapatia watoto wa kike 50,000 fursa ya kuhudhuria skuli za msingi mwakani.~~