Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ziara ya Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji nchini Tanzania

Ziara ya Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji nchini Tanzania

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) anazuru Tanzania hivi sasa. Kwa mujibu wa Msemaji wa UNHCR, Guterres anatarajiwa kuanzisha mradi wa miaka miwili nchini Tanzania uliokusudiwa kuhitimisha lile tatizo kongwe la wahamiaji karibu 218,000 wa kutoka Burundi waliopo Tanzania, umma ambao ulihama nchi baada ya machafuko ya 1972 kwenye maeneo yao.~