Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNODC yatahadharisha:'tatizo la madawa ya kulevya limedhibitiwa lakini halijasuluhishwa.'

UNODC yatahadharisha:'tatizo la madawa ya kulevya limedhibitiwa lakini halijasuluhishwa.'

Antonio Maria Costa, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Udhibiti wa Madawa ya Kulevya na Uhalifu (UNODC) alipohutubia kikao cha 51 Kamisheni ya UM dhidi ya Madawa ya Kulevya kilichokutana Ijumatatu Vienna – taasisi ambayo huzingatia sera za kukomesha janga la madawa haribifu duniani – alisema kwamba wakati umeshawadia kwa jumuiya ya kimataifa kuzingatia hatua ziada za kudhibiti vyema afya ya watu waliodhurika na madawa maovu badala ya kulenga huduma zake kudhibiti uhalifu pekee wa madawa ya kulevya.