Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uzuizi wa kihorera, askari wa kukodiwa na taka za sumu kusailiwa na BHB

Uzuizi wa kihorera, askari wa kukodiwa na taka za sumu kusailiwa na BHB

Baraza la UM juu ya Haki za Binadamu (BHB) limekutana mjini Geneva Ijumatatu kuzingatia ripoti tatu muhimu: awali, ripoti kuhusu taathira mbaya ya afya kutokana na utupaji haramu wa mabaki ya bidhaa za sumu, hususan katika mataifa yanayoendelea; pili, ripoti juu ya uzuizi wa kihorera unaowanyima watuhumiwa fursa ya kufikishwa mahakamani kuhukumiwa na, tatu, Baraza limezingatia ripoti kuhusu matumizi ya askari wa kukodiwa ambao hutumia mabavu kuuzuia umma usitekeleze haki yao halali ya kujiamulia wenyewe. ~~