Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ajira ya askari wa kukodiwa ni lazima idhibitiwe kisheria - UM

Ajira ya askari wa kukodiwa ni lazima idhibitiwe kisheria - UM

Baraza la Haki za Binadamu linalokutana hivi sasa mjini Geneva Ijumatatu lilizingatia ripoti ya UM iliyotoa onyo ya kwamba kunahitajika kidharura kudhibiti kisheroa zile kampuni za binafsi, zinazoendelea kuenea na kuongezeka kila siku ulimwenguni, ambazo huajiri polisi na wanajeshi wa kukodiwa. Iligundulikana kampuni hizi huendeleza shughuli zao kitaifa na kwenye maeneo yenye uhasama, kama Afghanistan, Iraq na Colombia bila ya kuheshimu kanuni za kimataifa kwa sababu imedhihirika yanapokiuka sheria, huwa hakuna wa kuyakosoa, na wala hayafanyiwi mapitio ya shughuli zao, na hawajibiki kwa matendo yao yasiofuata sheria za kimataifa. ~