Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msumbiji yafadhiliwa misaada ya dharura baada ya madhara ya Tufani Jokwe

Msumbiji yafadhiliwa misaada ya dharura baada ya madhara ya Tufani Jokwe

Mashirika ya UM juu ya maendeleo ya watoto (UNICEF) na miradi ya chakula (WFP) hivi sasa yanashiriki kwenye huduma za dharura za kusaidia umma wa Msumbiji kihali. Majuzi Tufani Jokwe, iliopiga eneo la kati na kaskazini ya taifa ilisababisha uharibu mkubwa wa zaidi ya nyumba 8,000 kwenye sehemu za mwambao na kuathiri watu 40,000 waliolazimika kungo\'lewa makwao.