Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF yahudumia kidharura waathiriwa wa Tufani Ivan Bukini

UNICEF yahudumia kidharura waathiriwa wa Tufani Ivan Bukini

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo ya Watoto (UNICEF) limo mbioni kuifadhilia Bukini huduma za kihali, baada ya Tufani Ivan Maututi kupiga kwenye eneo hilo mwezi uliopita, na kuangamiza makazi ya watu karibu 200,000. Hivi sasa UNICEF inafadhilia makumi elfu ya waathiriwa madawa, vyandarua, mablangeti pamoja na vifaa vya huduma ya afya.