Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama ya ICTR kuongeza hukumu kwa padri wa zamani Rwanda

Mahakama ya ICTR kuongeza hukumu kwa padri wa zamani Rwanda

Mahakama ya Rufaa ya ile Mahakama Kuu ya Kimataifa juu ya Rwanda (ICTR) iliopo Arusha, Tanzania imerekibisha hukumu yake ya hapo kabla na kuongeza adhabu kwa aliyekuwa padri wa madhehebu ya Kikatoliki nchini Rwanda, Athanase Seromba ambaye katika mwaka 2006 alihukumiwa kifungo cha miaka 15, kwa kusaidia na kuchochea mauaji ya karibu raia 1,500 wenye asili ya KiTutsi ambao katika 1994 walikimbilia ndani ya kanisa alikuwa akiliongoza kupata hifadhi katika mkoa wa Kibuye.