Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNEP inakhofu majabali ya barafu duniani yanayeyuka kwa kasi

UNEP inakhofu majabali ya barafu duniani yanayeyuka kwa kasi

Taasisi ya Utafiti wa Hali ya Majabali ya Mabarafu Duniani iliopo kwenye Chuo Kikuu cha Zurich, Uswiss na na ambayo huungwa mkono na Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) imeripoti kuwa baina ya miaka ya 2004 hadi 2006, majabali haya ya barafu yameonekana kuyayuka kwa kasi iliozidi mara mbili kiwango cha wastani, kutokana na athari haribifu za mabadiliko ya hali ya hewa duniani. Majabali haya ya barafu ni chanzo muhimu cha maji kwa mabilioni ya umma wa kimataifa.