Ripoti ya uzuiaji wa mauaji ya halaiki inasailiwa Geneva
Ijumatatu, Baraza la UM juu ya Haki za Binadamu mjini Geneva lilipokea ripoti mbili maalumu kutoka wataalamu wanaohusika na kinga na hifadhi ya wanadamu dhidi ya mauaji ya halaiki, pamoja na ripoti inayozingatia utekelezaji wa haki za binadamu katika Sudan.