Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bukini imetia sahihi ya kuridhia Mkataba wa Roma

Bukini imetia sahihi ya kuridhia Mkataba wa Roma

Mapema wiki hii taifa la Bukini limetia sahihi ya kuridhia Mkataba wa Roma, ambao ndio ulioanzisha Mahakama ya Kimataifa ya ICC. Mahakama ya ICC ni mahakama huru na ya kudumu, iliyodhaminiwa na jumuiya ya kimataifa madaraka ya kuhukumu wale watu waliotuhumiwa kufanya makosa mabaya ya jinai, mathalan, mauaji ya halaiki, jinai ya vita na vile vile yale makosa ya uhalifu dhidi ya utu.