Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO inahimiza kuongezwe juhudi za kupambana na TB Duniani

WHO inahimiza kuongezwe juhudi za kupambana na TB Duniani

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa ripoti mpya yenye mada isemayo Udhibiti wa Maradhi ya Kifua Kikuu (TB) Duniani 2008. Ripoti ilibainisha ya kuwa watu milioni 9.2 walipatwa na maradhi ya kifua kikuu katika 2006, idadi ambayo ilijumuisha, vile vile, watu 700,000 waliokuwa na virusi vya UKIMWI, pamoja na watu 500,000 ziada walioelemewa na kuugua TB sugu inayokataa hata ile tiba maarufu ya madawa ya mchanganyiko.~~

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.