Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Arbour kuyahimiza mataifa yaridhie Mkataba wa Kuondosha Ubaguzi Duniani

Arbour kuyahimiza mataifa yaridhie Mkataba wa Kuondosha Ubaguzi Duniani

Louise Arbour, Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya Utekelezaji wa Haki za Binadamu Duniani ametoa mwito maalumu kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Kufyeka Ubaguzi, mwito ambao umependekeza kwa Mataifa Wanachama kuidhinisha haraka ule Mkataba wa Kimataifa wa 1969 wa Kuondosha Aina Zote za Ubaguzi Ulimwenguni, na kujitahidi kuimarisha sheria zao kitaifa ili kuhakikisha waathiriwa wa janga la ubaguzi huwa wanapatiwa haki. Siku ya Kimataifa Kuondosha Ubaguzi huadhimishwa kila mwaka na jamii ya UM katika tarehe 21 Machi.~