Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baadhi ya wajumbe wa BU hawakufurahika na juhudi za upatanishi Myanmar

Baadhi ya wajumbe wa BU hawakufurahika na juhudi za upatanishi Myanmar

Baadhi ya mabalozi wa nchi wanachama katika Baraza la Usalama (BU) wamenakiliwa kuonyesha kuwa na masikitiko makubwa juu ya mzoroto wa zile juhudi za karibuni za upatanishi katika Myanmar zilizoongozwa na Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kwa Myanmar, Ibrahim Gambari. Lakini hata hivyo, wajumbe hawa waliahidi kwamba wataendelea kulimurika suala la Myanmar kwenye mijadala yao ili kuhakikisha linapatiwa suluhu ya kuridhisha na ya haki yenye masilahi kwa umma.