Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali Usomali inajadiliwa na Baraza la Usalama

Hali Usomali inajadiliwa na Baraza la Usalama

Baraza la Usalama leo linajadilia suala la Usomali kwa kusikiliza ripoti ya Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu kwa Usomali, Ahmedou Ould-Abdallah kuhusu maendeleo yaliopatikana katika wiki za karibuni katika kurudisha usalama, amani na upatanishi miongoni mwa yale makundi yanayohasimiana.