Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Ni dhamana ya walimwengu kuufyeka kipamoja ubaguzi', anasihi KM

'Ni dhamana ya walimwengu kuufyeka kipamoja ubaguzi', anasihi KM

Tarehe 21 Machi huadhimishwa na UM kuwa ni Siku ya Kimataifa Kuondosha Ubaguzi; na kwenye risala ya kuiheshimu siku hiyo, Katibu Mkuu Ban Ki-moon alikumbusha tena kwamba sera za ubaguzi hazijatoweka bado na zinaendelea kudhuru watu binafsi na jamii kadha wa kadha katika sehemu mbalimbali za dunia. Kwa hivyo, alizinasihi nchi zote wanachama, pamoja na makundi ya jumuiya za kiraia, halkadhalika, kuongeza juhudi zao na michango yao ili kuhakikisha tunadhibiti vyema zaidi ukabila na ubaguzi wa rangi kote ulimwenguni.