Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF yahitaji msaada wa dharura kwa waathiriwa mafuriko Namibia

UNICEF yahitaji msaada wa dharura kwa waathiriwa mafuriko Namibia

UNICEF imetoa ombi linalotaka ifadhiliwe msaada wa dharura wa dola milioni 1.2 ili kufarajia misaada ya kiutu kwa watu 65,000 waliopo eneo la Namibia kaskazini, umma ambao makazi yao yaliangamizwa na mvua kali zilizonyesha katika miezi ya Januari na Februari mwaka huu. Mvua hizi zilikiuka kiwango cha kawaida na zilisababisha mafuriko yaliogharikisha mastakimu kadha wa kadha nchini humo.