Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM inawakumbuka wafanyakazi walioghibiwa na hali ya hatari

UM inawakumbuka wafanyakazi walioghibiwa na hali ya hatari

Tarehe 25 Machi hutambuliwa na UM kuwa ni Siku ya Ushikamano wa Kimataifa Kuwakumbuka Wafanyakazi wa UM, Waume kwa Wake, Waliowekwa Vizuizini na Waliopotea wakati wakitumikia “maadili ya kiutu” katika sehemu mbalimbali za dunia. Risala ya KM kuadhimisha siku hii ilidhihirisha kwamba wafanyakazi wa UM 40, wingi wao wakiwa wazalendo, wameripotiwa kuwekwa vizuizini katika mataifa mbalimbali, na wengine wamekamatwa na baadhi yao wamepotea na kutoweka bila kujulikana walipo au walipohamishiwa. ~~