Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vurugu la Mashariki ya Kati laitia wasiwasi Baraza la Usalama

Vurugu la Mashariki ya Kati laitia wasiwasi Baraza la Usalama

Baraza la Usalama limekutana kwenye kikao cha hadhara Ijumanne kuzingatia na kusailia hali inayoendelea kuharibika katika Mashariki ya Kati. Naibu KM juu ya Masuala ya Kisiasa, Lynn Pascoe alipohutubia Baraza la Usalama aliwaambia wajumbe wa taasisi hiyo kwamba tangu alipowakilisha ripoti yake mwezi uliopita, kuhusu hali ardhini katika eneo zima la Mashariki ya Kati, juhudi za upatanishi zimeonekana kupwelewa, kwa sababu ya kuongezeka kwa vitendo vya utumiaji nguvu ambavyo vilisababisha idadi kubwa ya raia kujeruhiwa na kuuawa, hususan kwenye yale maeneo yaliokaliwa kimabavu katika Tarafa ya Ghaza, Ufukwe wa Magharibi ya Mto Jordan, baadhi ya maeneo ya Israel na nchini Lebanon.~