Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Karibu watu milioni wamedhurika mwaka huu na mafuriko, vimbunga kusini mwa Afrika - UM

Karibu watu milioni wamedhurika mwaka huu na mafuriko, vimbunga kusini mwa Afrika - UM

Ripoti mpya ya Ofisi ya UM inayohusika na Misaada ya Dharura Dunaini (OCHA) imeeleza ya kuwa watu karibu milioni moja wanaoishi katika mataifa ya Kusini mwa Afrika walisumbuliwa na kudhurika kihali mwaka huu kwa sababu ya mvua kali zisio za kawaida ambazo zilisababisha mafuriko na vimbunga haribifu.