Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Polio yaweza kudhibitiwa sehemu zote za dunia', asisitiza Mkurugenzi wa WHO

'Polio yaweza kudhibitiwa sehemu zote za dunia', asisitiza Mkurugenzi wa WHO

Mkurugenzi wa Ofisi ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa Ukanda wa Mediterranean ya Mashariki, Dktr Hussein Gezairy amenakiliwa akisema ya kuwa “mafanikio ya huduma za kuondosha polio Usomali yamethibitisha kwamba maradhi haya yanaweza kukomeshwa katika sehemu zote za dunia, hata kwenye yale maeneo yalioshuhudia vurugu na uhasama”, pindi jumuiya ya kimataifa itanuia kushirikiana kipamoja kuitekeleza miradi hiyo ya kudhibiti afya ya jamii. Hivi sasa ni mataifa manne tu duniani ambayo bado yanasumbuliwa na tatizo la polio ulimwenguni – mataifa hayo ni Afghanistan, India, Nigeria na Pakistan.