Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mafanikio ya kukomesha maradhi ya polio Usomali

Mafanikio ya kukomesha maradhi ya polio Usomali

Taasisi Inayohusika na Mradi wa Kuondosha Maradhi ya Kupooza/Polio Duniani (GPEI) imetangaza ya kuwa walimwengu, wiki hii, wamefikia ‘mafanikio ya kihistoria’ kuhusu afya ya jamii nchini Usomali, baada ya kubainika kwamba tangu tarehe 25 Machi 2007 hakujasajiliwa mgonjwa hata mmoja aliyeambukizwa na virusi vya maradhi ya polio katika taifa hilo.