Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU lazingatia ujenzi wa amani Guinea-Bissau

BU lazingatia ujenzi wa amani Guinea-Bissau

Baraza la Usalama (BU) limekutana, kwanza, kwenye kikao cha hadhara kuzingatia hali katika Guinea-Bissau, kufuatia ripoti ya karibuni ya KM iliyosailia hatua za kuchukuliwa kimataifa kulisaidia taifa hili la Afrika Magharibi kufufua tena huduma zake za maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na pia kijamii. Mwakilishi wa KM katika Guinea-Bissau, Shola Omoregie aliwaelezea wajumbe wa Baraza kwamba Ijumanne (25 Machi) usiku Raisi Vieira ametangaza kwamba Guinea-Bissau itafanya uchaguzi wa Baraza la Kutunga Sheria mnamo tarehe 16 Novemba. Tangazo hili, aliendelea kusema, linatarajiwa kuteremsha hali ya wasiwasi iliyolivaa taifa katika siku za karibuni, na alitumai washirika wenzi kutoka jumuiya ya kimataifa wataifadhilia Guinea-Bissau misaada inayohitajika kuendesha uchaguzi kwa utaratibu wa kuridhisha.