Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Haiwafalii Ghana kuhamisha kwa mabavu wahamiaji wa Liberia', yanasihi UNHCR

'Haiwafalii Ghana kuhamisha kwa mabavu wahamiaji wa Liberia', yanasihi UNHCR

Ofisi ya UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) imewanasihi wenye madaraka Ghana kujitahidi kusitisha haraka uhamisho wa nguvu kwa wahamiaji wa Liberia. Nasaha hii ilitangazwa baada ya Ghana kuamua Ijumapili kuwaondosha nchini wahamiaji 16 ambao walirejeshwa makwao kwa mabavu, kinyume na kanuni za kimataifa. Wingi wa wahamiaji hawa walikuwa wamesharajisiwa na UM wakisubiri kufarijiwa mahitaji yao ya kihali na UNHCR.