Skip to main content

'Uekezaji katika shughuli za maji hufaidisha kilimo Afrika, ukitekelezwa', kusisitiza mashirika juu ya maendeleo

'Uekezaji katika shughuli za maji hufaidisha kilimo Afrika, ukitekelezwa', kusisitiza mashirika juu ya maendeleo

Taasisi tatu zinazohusika na huduma za maendeleo - yaani Benki Kuu ya Dunia, Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) na pia Taasisi ya Ushirikiano Mpya wa Maendeleo ya Afrika (NEPAD) - ambazo zinakutana hivi sasa Tunis, Tunisia kuhudhuria Wiki ya Maendeleo ya Huduma za Maji Afrika, zimetoa mwito wa pamoja unaohimiza wahisani wa kimataifa kukithirisha msaada wao wa fedha zinazohitajika, kidharura, kufadhilia Usimamizi Bora wa Matumizi ya Maji kwa Kilimo katika Afrika, hasa kwenye miradi ya kutunza maji ya mvua, udhibiti bora wa mabomba ya maji na, pia, kilimo cha umwagiliaji maji.