Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Matokeo ya Malengo ya Milenia Duniani ni ya mchanganyiko, asema NKM Migiro

Matokeo ya Malengo ya Milenia Duniani ni ya mchanganyiko, asema NKM Migiro

Naibu KM (NKM) wa UM, Asha-Rose Migiro Alkhamisi alihutubia Mkutano wa Kuzingatia Hali ya Dunia kwa Sasa uliofanyika Chuo Kikuu cha Columbia, mjini New York ambapo alidhihirisha kwamba kumepatikana matokeo ya mchanganyiko kwenye zile juhudi za kimataifa za kukamilisha, kwa wakati, Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) yaliokusudiwa kupunguza umasikini kwa nusu katika nchi zinazoendelea itakapofika 2015.