28 Machi 2008
Naibu KM (NKM) wa UM, Asha-Rose Migiro Alkhamisi alihutubia Mkutano wa Kuzingatia Hali ya Dunia kwa Sasa uliofanyika Chuo Kikuu cha Columbia, mjini New York ambapo alidhihirisha kwamba kumepatikana matokeo ya mchanganyiko kwenye zile juhudi za kimataifa za kukamilisha, kwa wakati, Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) yaliokusudiwa kupunguza umasikini kwa nusu katika nchi zinazoendelea itakapofika 2015.