Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Haki za Binadamu limesihi Mataifa kutotumia ubaguzi wa rangi kupiga vita ugaidi

Baraza la Haki za Binadamu limesihi Mataifa kutotumia ubaguzi wa rangi kupiga vita ugaidi

Alkhamisi wajumbe 47 wanachama wa Baraza la Haki za Binadamu walipitisha Geneva maazimio sita muhimu kuhusu taratibu za kuimarisha haki za kimsingi za binadamu duniani. Miongoni mwa maazimio hayo muhimu lilikuwemo pendekezo maalumu liliopitishwa, kwa kauli moja, na bila ya kura, ambalo lilionya Mataifa Wanachama yote dhidi ya tabia ya kutafautisha kisheria watu, kwa sababu ya jadi, asili, dini au kabila, kwa kisingizio ya kupiga vita ugaidi.