Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Watoto wadogo bado wanaendelea kuajiriwa kupigana

Watoto wadogo bado wanaendelea kuajiriwa kupigana

Ripoti mpya ya KM juu ya hali ya watoto katika maeneo yenye mapigano imebainisha kwamba kuna baadhi ya nchi wanachama ambazo bado zinaendeleza karaha ya kuwalazimisha watoto wadogo kujiunga na makundi ya wanamgambo na kushiriki kwenye mapigano. Mataifa haya, kwa mujibu wa ripoti ya UM, hujumuisha Afghanistan, Burundi, Chad, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Colombia na vile vile Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Myanmar, Nepal, Philippines, Somalia, Sudan pamoja na Sri Lanka na Uganda.