Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM azuru makumbusho ya Mauaji ya Halaiki Rwanda

KM azuru makumbusho ya Mauaji ya Halaiki Rwanda

KM Ban alikuwepo Kigali, Rwanda mwanzo wa wiki na alizuru Makumbusho ya Mauaji Makubwa ya Halaiki. Alisema alihuzunishwa sana na aliyoyashuhudia, na alitoa mchango binafsi wa dola 10,000 kufadhilia mfuko wa Serikali ambao hutumiwa kuwasaidia mamia ya watoto mayatima wa mauaji hayo kupata elimu.