Operesheni za amani Ethiopia/Eritrea zaongezewa muda na Baraza la Usalama
Baraza la Usalama, kwa kauli moja, limepitisha azimio la kuongeza muda wa operesheni za amani mipakani Ethiopia na Eritrea kwa miezi sita zaidi, kwa sababu imeripotiwa hali ya wasiwasi bado inaendelea kukithiri kwenye lile eneo la kusitishwa mapigano la TSZ. Mataifa haya mawili vile vile yalinasihiwa kuondosha haraka vikosi vyao ambavyo hivi sasa vimeenezwa kwenye eneo la mgogoro la TSZ.