Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM na Rais wa Sudan waafikiana kuharakisha uenezaji wa vikosi vya amani Darfur

KM na Rais wa Sudan waafikiana kuharakisha uenezaji wa vikosi vya amani Darfur

KM Ban Ki-moon alipohudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika Addis Ababa, Ethiopia alipata fursa ya kukutana kwa muda wa saa na nusu na Raisi Omar al-Bashir wa Sudan, na waliafikiana umuhimu wa kuharakisha kupelekwa vikosi vya ulinzi wa amani vya UNAMID katika Darfur.