KM na Rais wa Sudan waafikiana kuharakisha uenezaji wa vikosi vya amani Darfur
KM Ban Ki-moon alipohudhuria Mkutano Mkuu wa Umoja wa Afrika Addis Ababa, Ethiopia alipata fursa ya kukutana kwa muda wa saa na nusu na Raisi Omar al-Bashir wa Sudan, na waliafikiana umuhimu wa kuharakisha kupelekwa vikosi vya ulinzi wa amani vya UNAMID katika Darfur.