Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahojiano juu ya CSD na mjumbe wa Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola

Mahojiano juu ya CSD na mjumbe wa Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola

Neema Buhile, ni mwakilishi wa Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola kutokea Tanzania ambaye yupo Makao Makuu akihudhuria kikao cha mwaka cha ile Kamisheni ya UM kuhusu Maendeleo ya Jamii (CSD). Muktadha wa kikao cha safari hii ulilenga zaidi kwenye masuala yanayofungamana na ajira, ulemavu, hali ya kuzeeka na pia vijana.