Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNAMID yaidhinisha na Sudan makubaliano kuhusu operesheni za amani Darfur

UNAMID yaidhinisha na Sudan makubaliano kuhusu operesheni za amani Darfur

KM wa UM Ban Ki-moon ametangaza kufanikiwa kutia sahihi Maafikiano ya kuidhinisha Hadhi ya Vikosi Mseto vya UM/UA vinavyotazamiwa kulinda Amani katika Darfur, mapatano yatakayojulikana kama Maafikiano ya SOFA. Rodolphe Adada, Mjumbe Maalumu wa UM/UA wa Shirika la Ulinzi wa Amani kwa Darfur, UNAMID alitia sahihi Muwafaka huu pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Deng Alor.