UNAMID yaidhinisha na Sudan makubaliano kuhusu operesheni za amani Darfur

UNAMID yaidhinisha na Sudan makubaliano kuhusu operesheni za amani Darfur

KM wa UM Ban Ki-moon ametangaza kufanikiwa kutia sahihi Maafikiano ya kuidhinisha Hadhi ya Vikosi Mseto vya UM/UA vinavyotazamiwa kulinda Amani katika Darfur, mapatano yatakayojulikana kama Maafikiano ya SOFA. Rodolphe Adada, Mjumbe Maalumu wa UM/UA wa Shirika la Ulinzi wa Amani kwa Darfur, UNAMID alitia sahihi Muwafaka huu pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan, Deng Alor.