Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Fafanuzi za Mjumbe wa Tanzania juu ya kikao cha Kamisheni ya CSD

Fafanuzi za Mjumbe wa Tanzania juu ya kikao cha Kamisheni ya CSD

Naibu KM Asha-Rose Migiro alifungua rasmi kikao cha 46 Kamisheni ya CSD wiki iliopita ambapo alitilia mkazo kwenye hotuba yake juu ya “jukumu muhimu la ajira na kazi stahifu katika kukuza maendeleo”, hususan kwenye nchi zinazoendelea. Ernest Ndimbo, Mkurugenzi wa Ajira kwenye Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Watoto Tanzania alikuwa miongoni mwa wawakilishi waliohudhuria mkutano wa Kamisheni ya CSD. Ndimbo alifanya mahojiano maalumu na Redio ya UM ambapo alichukua fursa hiyo kutupatia fafanuzi zake kuhusu kikao cha mwaka huu cha Kamisheni ya CSD.~