Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mjumbe wa vijana asailia kikao cha CSD juu ya maendeleo

Mjumbe wa vijana asailia kikao cha CSD juu ya maendeleo

Neema Buhile, ni mwakilishi wa Vijana wa Nchi za Jumuiya ya Madola kutokea Tanzania ambaye hivi majuzi alikuwepo hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa (UM) kuhudhuria kikao cha mwaka cha Kamisheni juu ya Maendeleo ya Jamii (CSD). Muktadha wa mkutano huo wa mwaka ulilenga zaidi yale masuala yanayofungamana na ajira, ulemavu, hali ya kuzeeka na pia vijana. Redio ya UM ilipata fursa ya kuzungumza na Neema ambaye alitupatia maoni yake kuhusu ushirikiano unaofaa kuendelezwa na wajumbe wa kimataifa ili kuyatekeleza mapendekezo ya vikao vya kimataifa, kama kikao cha mwaka CSD, kwa mafanikio. ~~Sikiliza mahojiano kamili kwenye idhaa ya mtandao.