Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Aliyekuwa Waziri Rwanda akana tuhumu za mauaji ya halaiki

Aliyekuwa Waziri Rwanda akana tuhumu za mauaji ya halaiki

Ijumanne Callixte Nzabonimana, aliyekuwa Waziri wa Vijana na Michezo wa Rwanda katika 1994 alikamatwa na wernye madaraka mkoani Kigoma, Tanzania na kuhamishiwa Arusha siku hiyo hiyo Arusha kwenye magereza ya Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR). Ijumatano alipofikishwa mahakamani mbele ya Jaji Dennis Byron alikana mashtaka 11 ya kushiriki kwenye mauaji ya halaiki Rwanda mnamo 1994, pamoja na tuhumu za kuandaa mazingira ya ukatili na kuchochea raia kushiriki kwenye vitendo haramu hivyo ambavyo vilikiuka Mikataba ya Geneva juu ya Hifadhi ya Raia kwenye Vita na Mapigano.