Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yataka ifadhiliwe dola milioni 34 kusaidia wahamiaji wa Burundi katika Tanzania

UNHCR yataka ifadhiliwe dola milioni 34 kusaidia wahamiaji wa Burundi katika Tanzania

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limetoa ombi la kutaka lifadhiliwe dola milioni 34 na jumuiya ya kimataifa kwa madhumuni ya kukamilisha mpango wa kuwapatia mastakimu ya kudumu wahamiaji 218,000 wa Burundi, wanaoishi kwenye kambi ziliopo kwenye mikoa ya Rukwa na Tabora, Tanzania tangu 1972 walipohajiri makwao kujiepusha na vurugu liliozuka nchini kutokana na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe. Ratiba ya mpango huo inazingatiwa na serikali za Tanzania na Burundi pamoja na UNHCR jkwa lengo la kusuluhisho tatizo la muda mrefu la wahamiaji wa Burundi katika Tanzania.