Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali katika Darfur Magharibi yazidi kuharibika

Hali katika Darfur Magharibi yazidi kuharibika

Ripoti ya KM iliyowakilishwa mbele ya Baraza la Usalama kuzingatia matayarisho ya kupeleka na kukamilisha vikosi mseto vya UM/UA kulinda amani Darfur, yaani vikosi vya UNAMID imebainisha ya kuwa hali katika Darfur Magharibi imezidi kuharibika katika miezi miwili iliopita, kitendo ambacho pia huzorotisha sana zile huduma za dharura zinazohitajika kufadhilia umma misaada ya kihali ili kunusuru maisha.