Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM utaisaidia Bukini kukabiliana vyema na athari za matofani

UM utaisaidia Bukini kukabiliana vyema na athari za matofani

UM hivi sasa unaisadia Bukini kukabiliana na hasara kuu iliozushwa na Tufani Ivan ambayo mapema wiki hii ilipiga mwambao wa mashariki-kaskazini ya taifa hilo la Bahari ya Hindi. Bukini, ikisaidiwa na mashirika ya UM sasa wanaandaa kipamoja huduma za dharura za kuukinga umma na kimbunga kingine chenye jina la Tufani Hondo, ambayo tumearifiwa ipo njiani ikielekea eneo la mashariki.