Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO itakithirisha misaada kwa waathiriwa wa mafuriko Kusini mwa Afrika

FAO itakithirisha misaada kwa waathiriwa wa mafuriko Kusini mwa Afrika

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limejiandaa kuongeza huduma zake kwa watu muhitaji milioni moja wanaoishi katika Malawi, Msumbiji, Zambia na Zimbabwe ambao waliathiriwa na uharibifu uliotifuliwa karibuni na mvua kali zilizozusha mafuriko yaliogharikisha mavuno na makazi. Kadhalika wapimaji wahali ya hewa wanaashiria mvua hizo zitaselelea kieneo hadi mwisho wa Machi, na wanakhofia zitauchochea Mto Zambezi kufura na kukuza uharibifu ziada kwenye maeneo husika ya kusini mwa Afrika.