Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mazungumzo ya amani ya Uganda Kaskazini yabashiria matokeo ya kutia moyo

Mazungumzo ya amani ya Uganda Kaskazini yabashiria matokeo ya kutia moyo

Wawakilishi wa Serikali ya Uganda pamoja na wale wa kundi la waasi wa LRA, wanaokutana hivi sasa katika mji wa Juba, Sudan Kusini kujadilia mamsuala ya upatanishi na amani wamekubaliana kuunda idara maalumu ya mahakama kuu itakayodhaminiwa madaraka ya kusimamia mashtaka ya watuhumiwa wa jinai ya vita viliyoshtadi nchini mwao kwa miaka ishirini na moja.