Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM ameanzisha rasmi kampeni ya kimataifa dhidi ya unyanyasaji wa wanawake

KM ameanzisha rasmi kampeni ya kimataifa dhidi ya unyanyasaji wa wanawake

Asubuhi ya leo, Ijumatatu, Februari 25, KM wa UM Ban Ki-moon alianzisha rasmi kampeni ya kimataifa ya kukomesha na kufyeka tabia ya kutumia mabavu na nguvu dhidi ya wanawake na watoto wa kike duniani. Kampeni ilitilia mkazo umuhimu na ulazima wa kukomesha kidharura vitendo vyote vya udhalilishaji wa kijinsia. Kampeni hii imeanzishwa siku ile ile ambapo Kamisheni ya UM juu ya Haki za Wanawake (CSW)ilipfungua rasmi, kwenye Makao Makuu ya UM, kikao cha mwaka, cha 52. Tutakupatieni taarifa zaidi juu ya Mkutano wa CSW hapo kesho. ~