Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Eritrea imekakamaa kuiwekea UNMEE vikwazo

Eritrea imekakamaa kuiwekea UNMEE vikwazo

Shirika la Ulinzi wa Amani Mipakani Ethiopia/Eritrea (UNMEE) limearifu kwamba wanajeshi wa Eritrea bado wanaendelea kuwaekea vikwazo dhidi ya shughuli zake. UNMEE ilitoa mfano wa kitendo kilichotukia juzi ambapo magari 8 ya UM yalizuiliwa kuelekea mji wa Asmara kukusanya vifaa vya uhamisho wa muda vya watumishi wa UNMEE waliotarajiwa kupelekwa taifa jirani la Ethiopia.